Ufunuo wa Yohana Mlango 22 Revelation

Ufunuo wa Yohana 22:1 Revelation 22:1

Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung'aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,

Ufunuo wa Yohana 22:2 Revelation 22:2

katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.

Ufunuo wa Yohana 22:3 Revelation 22:3

Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;

Ufunuo wa Yohana 22:4 Revelation 22:4

nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.

Ufunuo wa Yohana 22:5 Revelation 22:5

Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele.

Ufunuo wa Yohana 22:6 Revelation 22:6

Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

Ufunuo wa Yohana 22:7 Revelation 22:7

Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki.

Ufunuo wa Yohana 22:8 Revelation 22:8

Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.

Ufunuo wa Yohana 22:9 Revelation 22:9

Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.

Ufunuo wa Yohana 22:10 Revelation 22:10

Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

Ufunuo wa Yohana 22:11 Revelation 22:11

Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

Ufunuo wa Yohana 22:12 Revelation 22:12

Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Ufunuo wa Yohana 22:13 Revelation 22:13

Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

Ufunuo wa Yohana 22:14 Revelation 22:14

Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

Ufunuo wa Yohana 22:15 Revelation 22:15

Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Ufunuo wa Yohana 22:16 Revelation 22:16

Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi.

Ufunuo wa Yohana 22:17 Revelation 22:17

Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.

Ufunuo wa Yohana 22:18 Revelation 22:18

Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

Ufunuo wa Yohana 22:19 Revelation 22:19

Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.

Ufunuo wa Yohana 22:20 Revelation 22:20

Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu.

Ufunuo wa Yohana 22:21 Revelation 22:21

Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.